Nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka; nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa (Mwanzo 12:2-3).
Kutoka katika Biblia, tunaona hata katika umri wa uzee, Ibrahimu bado alikuwa tajiri, kwasababu Mungu alimbariki katika mambo yote. Alikuwa tajiri katika mifugo, fedha, na dhahabu (Mwanzo 13:2). Neno lililotafsiriwa, “mifugo” ni “wanyama wa shambani”; alikuwa na makundi ya mifugo, kondoo, mbuzi, n.k.
Alafu katika Mwanzo 24:1, bado tunasoma kitu kizuri kuhusiana na Ibrahimu; inasema, “Basi Ibrahimu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, na BWANA alikuwa amembariki Ibrahimu katika vitu vyote.” Maisha ya Ibrahimu yaliendelea kutokea utukufu hadi utukufu; hakukuwa na nyakati za kushuka chini. Huu ni mpango wa Mungu kwa maisha yako; kuelekea juu na mbele tu. Hataki ile hali ambapo, mahali fulani katika njia ya maisha yako, utasemwa kama yule aliyewahi kuwa tajiri; ameazimia usitawi wako ukawe wa milele.
U mtu mwenye haki wa Mungu, na Biblia inasema, “...njia ya wenye haki ni kama nuru ing’aayo, ikizidi kung’aa hata mchana mkamilifu” (Mithali 4:18). Hiyo ndiyo habari na maendeleo ya maisha ya yule aliye katika Kristo.
Hivyo, si tu kwasabu umestaafu basi ndio uwe fukara; Biblia inasema, “Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na Ibrahimu aliyekuwa mwenye imani” (Wagalatia 3:9). Umebarikiwa pamoja na Ibrahimu aliyekuwa mwenye imani, na katika ongezeko la mali na usitawi wako, hakutakuwako na mwisho! Ahimidiwe Mungu!
